Pilau ya Nyama na Mtindi - ChefMapishi.



Pilau Ya Nyama Na Mtindi

VIPIMO:


  • Nyama iliyokatwa vipande - 1 Ratili(LB)

  • Mchele Basmati - 2 Magi

  • Chumvi ya wali - kiasi

  • Kitungu kilichokatwa katwa - 1 kikubwa

  • Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi - 1 kijiko cha supu 

  • Mtindi (yogurt) - ½ kikombe

  • Mchanganyiko wa bizari ya pilau ya tayari - 2 vijiko vya supu

  • Mafuta kidogo yakukaangia

  • Rangi ya manjano (ukipenda)


Mpendwa Msomaji, tunakushauri kutumia APP yetu ili kusoma kwa urahisi MAFUNZO UPISHI.  Sasa inapatikana Playstore, ili ku-download BOFYA HAPA.



NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA:


  •  Osha mchele na roweka nusu saa .

  •  Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitungu mpaka viwe rangi ya hudhurungi (brown).

  • Tia saumu na tangawizi na ukaange kidogo.

  • Kisha weka bizari ya pilau halafu nyama huku unakaanga nyama isiwe nyekundu tena.

  • Tia maji gilasi 1½- 2 ichemke mpaka nyama iwive na karibu kukauka.

  • Mimina mtindi na iachie moto mdogo ikauke kidogo.

  • Kwenye sufuria nyingine chemsha mchele pamoja na chumvi na mafuta kidogo mpaka uive.

  • Mimina wali juu ya nyama, kisha nyunyiza rangi (ukipenda) kama vile wali wa biriani na ufunike kwa dakika kumi hivi.

  • Changanya  wali na nyama pamoja ikiwa tayari kuliwa.


Mpendwa Msomaji, tunakushauri kutumia APP yetu ili kusoma kwa urahisi MAFUNZO UPISHI.  Sasa inapatikana Playstore, ili ku-download BOFYA HAPA.

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post
Ads1
Ads2