Pilau ya Nyama Ng'ombe na Nyanya - ChefMapishi.








Jinsi ya Kupika Pilau Ya Nyama Ng'ombe Na Nyanya.

Vipimo.

  • Mchele (Basmati) - 3 vikombe
  • Nyama ya ngo’mbe - 1 kg
  • Pilipili boga - 1 kubwa
  • Nyanya - 2 kubwa
  • Vitunguu maji - 2 vikubwa
  • Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa - 1 kijiko cha supu
  • Tangawizi - 1 kijiko cha chai
  • Ndimu - 1
  • Mafuta ya kupikia - ½ kikombe
  • Mdalasini - ½  kijiko cha chai
  • Binzari nyembamba - 1 kijiko cha chai
  • Pilipili manga - ½ Kijiko cha chai
  • Hiliki - ½ Kijiko cha chai 

Mpendwa Msomaji, tunakushauri kutumia APP yetu ili kusoma kwa urahisi MAFUNZO UPISHI.  Sasa inapatikana Playstore, ili ku-download BOFYA HAPA.

Namna ya kutayarisha na Kupika.

Roweka mchele wako katika chombo

Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi

Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi

Katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni

Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia

Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto

Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya

Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi

Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke

Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza

Funika na punguza moto na uache uive taratibu

Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.


Mpendwa Msomaji, tunakushauri kutumia APP yetu ili kusoma kwa urahisi MAFUNZO UPISHI.  Sasa inapatikana Playstore, ili ku-download BOFYA HAPA.

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post
Ads1
Ads2