Ndizi (aina yeyote, katika mapishi haya nimetumia ndizi bukoba)
Karoti
Pilipili hoho
Vitunguu maji
Chumvi
Nyanya
Ndimu
Maelekezo
Menya ndizi na uhifadhi kwenye chombo chenye maji ili zisipate kubadilika rangi
Andaa samaki – osha, kata vipande vinavyofaa au kama unapenda mpike
mzima – kamulia ndimu. Changanya samaki na limao. Kisha mhifadhi samaki
pembeni.
Andaa nyanya – osha na kisha menya nyanya 3 na kuzikata vipande vidogo. Hifadhi kwenye chombo.
Menya vitunguu maji 2 vikubwa halafu kata kwenye vipande vidogo unavyopendelea.
Osha na kisha kata pilipili hoho 1 kubwa kwenye vipande vidogo. Fanya vivyo hivyo kwa carrots 1 kubwa
Weka ndizi kwenye sufuria au kikaangio kinachofaa kupikia
Weka vitunguu maji juu ya ndizi, halafu weka nyanya juu yake, kisha malizia na karoti.
Weka samaki wako kwenye kikaangio kwa kuwapanga vizuri juu ya karoti.
Nyunyizia chumvi ya kutosha. Usiongeze mafuta maana kwenye samaki na
vitunguu kuna mafuta ya kutosha, hivyo haina haja ya kuongeza zaidi.
Weka maji kiasi kama kikombe 1 kikubwa halafu funika na mfuniko
usioruhusu mvuke kutoka. Hii inasaidia zile mboga mboga (karoti,
pilipili hoho, kitunguu na nyanya) zichuje maji yake na kukipa chakula
radha na harufu nzuri.
Subiria kwa muda wa dakika 15 hadi 20 na mchemsho wako utakuwa tayari kuliwa.
Post a Comment